MBIO ZA KIROHO KATIKA KULIISHI KUSUDI LA MUNGU - LIFE IN JESUS MINISTRY

Breaking

LIVE GOD LIFE

live life in jesus

Post Top Ad

LIVE LIFE IN JESUS

Sunday, November 26, 2017

MBIO ZA KIROHO KATIKA KULIISHI KUSUDI LA MUNGU



1Wakorinto 9:24-26
Tunahitaji kupiga mbio za kiroho ili kuliishi kusudi  la Mungu ili tuweze kupokea taji.
    Mkristo au mwamini unatakiwa  kuishi maisha yanayolenga shabaha katika kusudi la Mungu ili uje kupokea taji.huwezi kufika mahala bila kuw mpinzani
                       Waefeso 1;11
Kusudi ndilo linalosabisha uwepo mahali ulipo,pasipo kusudi la Mungu usingekuwepo.Mungu anathamini kusudi kuliko maisha,Mazingira unayopitia anaweza kukuinua ili kuonesha kusudi la Mungu kwa watu.
     Wafilipi 3:6-12 
     Yeremia 1:4-8
Kusudi linabeba hatima ya maisha yakona kusudi ndilo limebeba ramani ya maisha yako haijalishi unakataliwa na watu,wala kukutenga ila  ni katika  kusudi la Mungu   kutimia na kujidhihirisha katika maisha yako.
 Isaya 49;1-3
NAWEZAJE KUPIGA MBIO ZA KIROHO KATIKA KULIISHI KUSUDI LA MUNGU? 
UFAHAMU WA KIMUNGU NDANI YAKO                                                            
 Kuwa na ufahamu wa kimungu katika  maisha yako kujenga mahusiano yako vizuri na Mungu  kunaweza kukufanya kuishi katika malengo na kusudi la kimungu ndani yako.Bidii yako katika kusoma neno la Mungu na kukaa vizuri na Mungu itakupa kujitambua.     Isaya 55:10-11  ,Yoshua 1;8
KUJIKANA NAFSI YAKO
 Kuacha mambo ambayo yanakufanya ushindwe kutimiza kusudi la Mungu kwa kupenda kitu fulani kinachoujaza moyo wako unatakiwa kuyaacha na kujenga mahusiano yako vizuri na Mungu
KUJITOA MHANGA                                                                                                                 
 Kujitoa kwa kila kitu katika kumtumikia Mungu kw mali,moyo,akili,na mengineyo kwwa ajili ya kujenga  ufalme wa mungu                                                    


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

LIVE LIFE IN JESUS